Aliyekuwa
mchezaji wa Borussia Mönchengladbach ambae pia ni raia wa Uswizi Granit Xhaka
sasa ni mchezaji rasmi wa Arsenal FC ya Uingereza.
Katika pita
pita zetu tumeweza kujipatia picha mpya zaidi ambazo hazijatolewa katika
mitandao yeyote zikionyesha Xhaka akipiga picha akiwa amevalia sare za msimu
ujao za Klabu ya Arsenal.
Raia huyo wa
Uswizi mwenye umri wa miaka 23 alitarajiwa kutia sahihi mkataba na The Gunners unaokisiwa
kugharimu Pauni Milioni 25 baada ya kutua jijini London siku ya Ijumaa, Mei 20.
Xhaka
anatarajiwa kuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na Arsenal katika dirisha hili
la uhamisho msimu wa kiangazi nchini Uingereza.
Hata hivyo tangazo rasmi la kukamilika kwa uhamisho huo
linatarajiwa kutolewa wakati wowte kuanzia sasa.
Ni habari
ambayo itawafurahisha mashabiki wengi wa klabu ya Arsenal kote duniani. Kulingana na
mwanahabari Jack Pitt-Brooke wa gazeti la Independent, Granit Xhaka ametua
jijini London hii leo kumalizia hatua zake za mwisho kabla ya kuhamia miamba wa
kambumbu wa EPL jijini Londo, Arsenal.
Nyota huyo
mwenye umri wa miaka 23 ambaye ameibuka kuwa kiungo matata barani Uropa amekuwa
akitajwa kwa muda mrefu kuwa mchezaji wa kwamba kusajiliwa na Klabu hio katika
dirisha kubwa la uhamisho nchini humo la msimu wa kiangazi.
Hata hivyo
kulitokea taarifa tata kuhusiana na kitita cha pesa ambacho Klabu ya Arsenal
iliweka mezani katika majadiliano ya kumnunua mchezaji huyo kutoka klabu yake
ya Borussia Mönchengladbach. Laini taarifa hizi kwamba ameshatua jijini London
basi zitawapa furaha nyingi mashabiki wa The Gunners.
Mapema wiki
hii Xhaka alitaja Klabu ya Arsenal kama klabu ambacho angependa muno
kukichezea.
Mashabiki wa Arsenal sasa wanasubiri kwa hamu kuona usajili huo
umekamilika huku Xhaka akitarajiwa kuipiga jeki ngome ya kiungo cha kati ya The
Gunners.
Msanii wa kike kutoka Marekani mwenye asili ya Barbados, Rihanna haachi
kuzua gumzo kila mara. Hili linatokea akiwa kazini ama hata akiwa kwenye
likizo.
Ijumaa iliyopita alizua hali tete baada yake kuhudhuria mechi ya
mpira wa vikapu jijini New York huku akiwa amevaa kitopu bila sidiria ndani.
Rihanna akishabikia Brooklyn Nets
Tendo hili kidogo lilizua tumbo joto kwenye mechi kati ya Brooklyn Nets na Toronto Raptors baada yake kuketi kwenye safu ya mbele pande ya mashabiki wa Brooklyn Nets
huku chuchu zake zikionekana kupinda na kuwazuzua sio mashabiki wa kiume pekee
bali hata wale wa kike.
Huku akiwa amevaa hipster iliyombana na kuitoa ile figa yake kati,
msanii huyo anayevuma na kazi yake mpya ya ‘Something More’ alionekana kupungwa
na jinsi Brooklyn Nets ilivyowalemea wenzao wa Toronto Raptors kwa vikapu 102
kwa 98.
Rihanna akiwa na rafiki wake wa karibu
Rihanna aliyejumuika na rafiki zake wawili alionekana wakati huo
wote akijiburudisha na kinywaji baridi labda sababu kuu yake ya kuvalia kivazi
kilichoonyesha sehemu cha chuchu zake.
Aidha msanii huyo aliyevuma na kazi yake ya ‘Umbrella’ alionekana
na kipochi kilichochorwa noti ya Dola Mia Moja ya Marekani ambacho
kinakakadiriwa kugharimu Dola 48 za marekani.
Rihanna
Kilichowashangaza wengi aidha ni kutokuwepo kwa mchumba wake,
Drake ambaye kwa siku za hivi majuzi wamekuwa wakiandamana kila sehemu kama mtu
na kivuli chake. Mara ya mwisho ya wawili hao kutokea kwenye umma wakiwa pamoja
ni wiki moja iliyopita walipokwenda kupata chajio kwenye mkahawa wa Madeo eneo la West Hollywood.
Riri kama anavyofahamika na wendani wake wa karibu yupo jikoni kwa
sasa akiandaa albam yake ya nane ya studio ambayo inapikwa na Maprodyusa DJ
Mustard, David Guetta na Nicky Romero.
Rihanna alizaliwa Februari, 20 mwaka 1988 kama Robyn Fenty katika
Parokia ya St. Michael, Barbados. Alisajiliwa kwenye rekodi za Def Jam akiwa na
umri wa miaka 16 pekee na kwenda kutoa albam yake ya kwanza mwaka wa 2005
iliyouza zaidi ya kopi milioni 2 duniani.
Habari
zilizogonga vichwa barani Afrika na dunia nzima kuhusu ugomvi ulioibuka wiki
iliyopita baina ya mapacha Peter and Paul kutoka nchini Naijeria wanaounda
kundi la P-Square na kaka zao ziliwashtua wengi ila hakuna mtu aliyejua kiini
cha sakata hio kilikuwa ni nini. Kulingana na chanzo kilichoko karibu na mapacha
hao kilitoa sababu kamili ya ugomvi huo.
Chanzo
hicho aidha kimedokeza kwamba mgogoro uliletwa na wasaidizi wao wa kibinafsi al
maaruf PA’s.
Ukoko
ulianza kualika maua pale Msaidizi wa kaka yao mkubwa Jude ajulikanaye kama
Wande alimpa Msaidizi wa Peter ajulikanaye kama Shege hela ili akamsajilie gari
lake lakini Shege alikosa kufanya hivyo na kuzitumia hela hizo kwa shughuli
zingine ambazo hazijabainika.
Baada
ya hapo inadaiwa kuwa Msaidizi wa Jude aligadhabishwa muno na tendo hilo la
Msaidizi wa Peter.
Jambo
hili lilimpeleka nyumbani kwa mapacha hao ijulikanayo kama ‘Squareville’ ili
aweze kukabiliana na Msaidizi wa Peter, Shege. Hapo ndipo ngoma ikachukua mwelekeo
mbovu. Mambo yalichachawa pale Peter alipoingilia mzozo huo na kutaka
kumpiga Msaidizi wa Jude, Wande. Pale Paul alipojaribu kumkanya, chanzo chetu
kinasema Peter alimkandamiza ngumi Paul hadi akaanguka. Paul aidha
hakumrudishia ngumi kakake na badala yake kaka yao mwingine anayejulikana kama
Tony aliingilia na kuanza kupigana na Peter.
Chanzo chetu aidha kimedai kiini cha vuta n’kuvute hii ni zaidi ya
sintofahamu hio na Wasaidizi wao. Aidha inadaiwa kwamba Peter amekuwa akifanya
kila awezalo aidha awe mhusika mkuu wa maswala ya kifedha ya kundi la P-Square
ama aweze kupata mgao mkubwa zaidi na kwa pande nyingine inadaiwa kwamba Paul
anasisitiza kwamba kaka yao mkubwa anayejulikana kama Jude ambaye ni Meneja wa
mapacha hao aendelee kuwa Msimamizi wao wa Maswala ya Kifedha.
Kipute
hiki kilinuka kiasi ya kwamba ndugu hao walitaka wagawane mali yao ili kitu
mmoja aende njia yake.
Lakini
baada ya purukushani hii iliyochukua siku kadhaa, Paul alipost hivi katika
ukurasa wake wa Facebook.
“After
the storm comes calm. Hoping for better days ahead as one family. God’s
intervention”.
Labda
hii ni ishara kwamba ndugu hao wameweka tofauti zao za kibinafsi kuhakikisha
kwamba jina la P-SQUARE litaendelea kung’aa duniani kama ilivyokuwa.
Sisi
hapa Tamashani tunawaombea kila la kheir katika maono yao.