Sunday, 27 April 2014

Rihanna; jamani ni joto, fesheni ama mitego tu..?

Rihanna 
Msanii wa kike kutoka Marekani mwenye asili ya Barbados, Rihanna haachi kuzua gumzo kila mara. Hili linatokea akiwa kazini ama hata akiwa kwenye likizo.
Ijumaa iliyopita alizua hali tete baada yake kuhudhuria mechi ya mpira wa vikapu jijini New York huku akiwa amevaa kitopu bila sidiria ndani.
Rihanna akishabikia Brooklyn Nets
Tendo hili kidogo lilizua tumbo joto kwenye mechi kati ya Brooklyn Nets na Toronto Raptors baada yake kuketi kwenye safu ya mbele pande ya mashabiki wa Brooklyn Nets huku chuchu zake zikionekana kupinda na kuwazuzua sio mashabiki wa kiume pekee bali hata wale wa kike.
Huku akiwa amevaa hipster iliyombana na kuitoa ile figa yake kati, msanii huyo anayevuma na kazi yake mpya ya ‘Something More’ alionekana kupungwa na jinsi Brooklyn Nets ilivyowalemea wenzao wa Toronto Raptors kwa vikapu 102 kwa 98.
Rihanna akiwa na rafiki wake wa karibu
Rihanna aliyejumuika na rafiki zake wawili alionekana wakati huo wote akijiburudisha na kinywaji baridi labda sababu kuu yake ya kuvalia kivazi kilichoonyesha sehemu cha chuchu zake.
Aidha msanii huyo aliyevuma na kazi yake ya ‘Umbrella’ alionekana na kipochi kilichochorwa noti ya Dola Mia Moja ya Marekani ambacho kinakakadiriwa kugharimu Dola 48 za marekani.
Rihanna
Kilichowashangaza wengi aidha ni kutokuwepo kwa mchumba wake, Drake ambaye kwa siku za hivi majuzi wamekuwa wakiandamana kila sehemu kama mtu na kivuli chake. Mara ya mwisho ya wawili hao kutokea kwenye umma wakiwa pamoja ni wiki moja iliyopita walipokwenda kupata chajio kwenye mkahawa wa Madeo eneo la West Hollywood.


Riri kama anavyofahamika na wendani wake wa karibu yupo jikoni kwa sasa akiandaa albam yake ya nane ya studio ambayo inapikwa na Maprodyusa DJ Mustard, David Guetta na Nicky Romero.
Rihanna alizaliwa Februari, 20 mwaka 1988 kama Robyn Fenty katika Parokia ya St. Michael, Barbados. Alisajiliwa kwenye rekodi za Def Jam akiwa na umri wa miaka 16 pekee na kwenda kutoa albam yake ya kwanza mwaka wa 2005 iliyouza zaidi ya kopi milioni 2 duniani.




No comments:

Post a Comment