Saturday, 19 April 2014

P-Square yasambaratika..?


P-Square



Baada ya mitandao ya kijamii nchini Naijeria kuchapisha habari kwamba mapacha, Peter na Paul wanaounda kundi la P-Square wanataka kutengana kutokana na kutoelewana, msemaji wa kundi hilo Bayo Adetu amejitokeza na kukanusha madai hayo.

Akiongea na Premium Times, Adetu alisema hivi na namnukuu,

“I am too busy to give some wanna be blogger traffic, I don’t know where that report is coming from. Maybe they just want to get traffic to their site. It’s baseless and untrue.”
 
P-Square

Bara zima la Afrika liliamkia habari hizi za kutamausha kuwa mapacha hao walitofautiana kiasi cha kutaka kupigana wakati wakiwa mazoezini.
 
P-Square wakiwa na kaka yao mkubwa na Maneja Jude Okoye
Kuchachawiza habari hizo zaidi, kaka ya P-Square, Jude Okoye ambaye ndie Maneja wao alitweet akisema, 

“After over 10 years of hard work, it’s over. Am done.”

Wengi walioona hii kuwa ishara kamili kwamba Jude amejitoa kutoka kwa kundi hilo baada ya kudai kuwa hatohudhuria ndoa ya kisasa ya mdogo wake itakayoandaliwa Dubai.
Duru za kuaminika pia zinatuarifu kwamba Jude Okoye hana uhusiano mwema na mke wa Peter Okoye, Lola Omotayo, jambo ambalo lilimfanya kutohudhuria harusi yao.


 
P-Square na wake zao

 

 


No comments:

Post a Comment