Friday, 18 April 2014

R.I.P Hip Hop eti..?



Kifo chatangazwa cha sanaa mnayoipenda Hiphop imeshindwa kumaliza calendar
 
Ni swala ambalo naamini litazua mitazamo tofauti. Je, mziki aina ya Hip Hop upo ama ushaaga? Ni swali ambalo limezungumziwa na Msanii wa Hip Hop Jemedari kutoka nchini Kenya ambaye anasimama na vina vya kina katika kazi yake mpya, R.I.P Hip Hop akisema kwamba ile real Hip Hop haipo tena duniani. Sikiliza kazi hio kupitia hino link.

https://www.youtube.com/watch?v=XmzyCLEr408
 
Kama ada yetu tulimtafuta Jemedari na kutaka kupata kauli yake kuhusiana na na swala hili. Na hivi na mazungumzo kwa njia ya chat yalivyokuwa.




Sylvano Mbatu
Vipi kaka. Kazi nzuri. Ila naomba unifafanulie mbona ukaamua kuimba R.I.P Hip Hop.
Unazungumzia nani kwenye beti zako?
Ni utunzi tu ama ni mtu flani aliyepitia hayo?
Ile 'old' generation ya wasanii ambao kiasi hawakufanikiwa kama tulivyotarajia
Anhaa
Kwanzia Kshaka na Ukoo Flani kwa ujumla. Ni kama sanaa ya hiphop ilikufa hapo kiasi..
Hadithi ni kwa ujumla tu lakini ni career za wasanii weni zimelengwa hapo..
Oh ok
So hivi wataka kuthibitisha kwamba hip hop imekufa?
Ile "old school" flavour ya kina Kshaka, kwa mfano, haipo tena..
New cats wamekuja na mitindo tofauti, ila ni vigumu kupata heshima kutoka kwa hawa wakongwe..
Oh ok
Hino flava mpya ambayo ipo sokoni kwa sasa, je waeza ipa jina gani? Hip Hop?
Ni hiphop, ile new school.
Kisha kuna Candy Rap, utani kisha mizani na utunzi mwepesi mno
Kina Camp Mulla, Jay A, na kadhalika..
Anhaa

So huo ndo mtazamo wa msanii Jemedari. Hapa Tamashani tukisubiri ujio wa kanda ya video ya kazi hii, tutazidi kutafuta mitizamo kutoka kwa wakali wa Hip Hop kutoka kwenye kanda hii tujue wanafeel aje.
Jemedari amekuwa katika mstari wa mbele katika kufanya sanaa ya Hip Hop san asana kwenye njia ya kutumia ala ama Live Performance. Vile vile amejihusisha na kuandaa tamasha za Hip Hop kama vile Suit n Mics.

No comments:

Post a Comment