Sunday, 20 April 2014

Niacheni Nidate’ asema Raz a.k.a Raz Swagg Level..!

Raz
Msanii wa kizazi kipya Raz a.k.a Raz Micha aitwavyo akiwa mtaani aonyesha kila sababu ya kwa nini yeye ni mojawapo ya wasanii wanaongoza fani ya mziki wa kizazi kipya kutoka Pwani ya Kenya baada ya kuachilia pini jipya na bonge la video linalokwenda kwa jina ‘Niache Nidate’.
Raz akiwa na Marie kwenye shoot ya 'Niache Nidate'

Kazi hio ilifuatiliwa na kuachiliwa sokoni kwa video kali iliyofanywa na muongozaji namba moja wa video eneo la Pwani ya Kenya Lil Guy G, video ambayo imeshirikisha wakali kibao wa kazi hizi kama vile, Ally Kiba, Sylvano Mbatu (Mkurugenzi wa Tamashani), Bob Junior a.k.a Sharobaro President na Bonge la Nyau kutoka nchini Tanzania bila kusahau mtoto wa kike Marie aliyeigizia kwenye kanda hio ambaye ni bonge la actress kwenye vipindi aina aina humu nchini.
Raz akila bata pamoja na Ally Kiba


Akizungumza na meza ya Tamashani, Raz ambaye majina yake rasmi ni Rama Sultan alihoji kwamba aliwekeza kitita kikubwa cha fedha kuhakikisha kwamba kazi hio imekubalika kwenye kanda hii.

Fidempa(kushoto), Prodyusa Totti pamoja na Raz wakiwa jikoni
Raz ameweza kutamba anga zake kama msanii mwenye umri mdogo ila mwingi wa ujuzi na ufundi... Hili limemwezesha kufanya kazi na wasanii kama vile Ally Kiba kwenye ‘Mjanja wa Jiji’, Hakim5 kwa 'Nidanganye', J.I kwenye 'Dini', Chikuzee, AT kwenye track 'Sina Habari na Mtu', CLD, Fidempa kwenye track ya 'Swagger Up', Lil Kizzy kutoka Germany, Wizzy A kutoka Naijeria na wasanii wengine kwenye kanda hii.

Sylva(Meneja wa Tamashani), Babyone(Msanii kutoka Sudan Kusini) pamoja na Raz.
Licha ya hayo bado ana maono kufanya kazi zingine kubwa na wasani tofauti wa kimataifa maana ana maono makubwa na kazi yake ..

Kwa sasa hapa Tamashani tunamtakia kila la Kheri na tunampa Raz nafasi ya Kudata maana wakati wake ndio sasa.

No comments:

Post a Comment